Fahamu Mwezi Sahihi Wa Kuyapanga Malengo Ya Kimafanikio Kabla Haujauanza Mwaka Mpya.

Zikiwa na siku kadhaa zimesalia ili kukamilisha mwaka na kuanza mwaka mpya ipo haja kubwa sana ya kufahamu mambo ya msingi yanayohusu malengo yako ambayo uliyapanga mwaka huu na jinsi ya kuanza vyema mwaka mpya ujao.

Fanya tafakari kuhusu malengo.

Chukua walau dakika chache kutafakari juu ya malengo ambayo ulijipangia mwaka jana  ni je umeyakamilisha kwa asilimia ngapi? na kama hujakamilisha ni nini kilikuwa kikwazo kikubwa kilichofanya usikamilishe malengo hayo?

Nakusihi ufanye zoezi hili  la tafakuri juu ya maisha yako ili ujue ni wapi ulipokosea na ufanye marekebisho, ili mwaka ujao usifanye makosa hayo hayo tena ambayo yatakusababisha ushindwe tena kutimiza malengo yako Utakayopanga kuyafanya mwaka ujao.
Katika suala la upangaji wa malengo watu wengi huwa tunakosea sana ila  naomba nikukumbushe ya kwamba katika upangaji wa malengo yako ya kimafanikio mwezi wa kwanza sio mwezi wa kupanga malengo yako bali uwe ni mwezi wa kutekeleza malengo ulikwishayapanga mwezi wa  12.

Hivyo kwa maneno mengine naomba nikupe fasihi hii, mwezi wa 12 ni mwezi wa kupanga malengo yako, inapofika mwezi 1 mpaka mwezi 11 uwe ni mwezi wa kutekeleza malengo hayo.

Mpaka kufikia hapo nikutakie upangaji mwema wa malengo yako katika mwezi huu wa upangaji malengo, huku ukiweka nguvu na akili katika utekelezaji hapo mwaka ujao.

Asante kwa kusoma fasihi hii nikutakie siku njema na mafanikio mema.

Ndimi: Afisa Mipango Benson Chonya.


Iklan Atas Artikel

Iklan Tengah Artikel 1

Iklan Tengah Artikel 2

Iklan Bawah Artikel