Ukifanya Kazi Zako Hivi, Huwezi Tena Kufanikiwa.

Acha Kufanya Kazi Kinyonge

Kama unafanya kazi yoyote ile acha kufanya kazi hiyo kinyonge, acha kufanya kazi hiyo kwa kuamini kwamba utaenda kupata matokeo hafifu au matokeo ya chini, fanya kazi yako kama mshindi na usiogope kitu.

Ukienda kufanya kazi yako kwa kuamini utashinda, basi utaweza kushinda kweli. Ni hatari sana kufanya kazi zako kinyonge kwa kuamini umeshindwa, kwa hiyo unafanya ili usukume siku, ogopa sana hiyo kitu maishani mwako. 

Watu wengi wanafanya kazi zao kwa mtazamo wa kinyonge, wanafanya kwa kuamini kwamba mambo yameishia hapo na hawawezi kufanikiwa pa kubwa, huo ni mtazamo hatari ambao unawapoteza kabisa.

Ili kufanikiwa, acha kabisa kufanya kazi kinyonge. Kazi yoyote ifanye kishujaa. Usiione ni kazi ya washindwaji, ona ni kazi ya kukufanikisha, na acha kuidharau hata kidogo inayokupa kula yako ya kila siku.

Ukiifanya kazi yako kishujaa na kuipa heshima, utafanikiwa.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

Iklan Atas Artikel

Iklan Tengah Artikel 1

Iklan Tengah Artikel 2

Iklan Bawah Artikel