Wakimbie Watu Hawa.

Kuna watu ambao wao wana asili ya ugumu tu. Ni watu ambao hawataki vyao vitumike, ila ni watu wanaopenda kutumia vya wengine. Hawa ni watu ambao kama wanyonyaji wa wengine.

Watu hawa ni wazuri sana katika kufurahi, na kucheka na vitu vya watu. Lakini inapofika vya kwao kutumiwa au kuliwa wanakuwa wagumu sana na hawataki hata kidogo kuguswa. 

Unapokuwa na watu kama hawa, jihadhari. Achana na marafiki kama hawa, ambao wao urafiki wao, unapokuwa na kitu, ukikosa kitu wanakutupa. Rafiki wa kweli ni yule akufaae kwa dhiki.

Kwa nini uwe na marafiki wanaotaka kukutumia tu na kukutupa unapokuwa huna kitu. Kataa hili, chagua rafiki bora ambao mnaendana. Achana na marafiki wanafiki maishani.


Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

Iklan Atas Artikel

Iklan Tengah Artikel 1

Iklan Tengah Artikel 2

Iklan Bawah Artikel