Umaskini Wako Unasababishwa Na Kitu Hiki Tu,...




Watu sio maskini eti kwa sababu hawana pesa, watu ni maskini ni kwa sababu ya mawazo yao. Unaweza ukawa unapato zuri sana lakini ukabaki kuwa maskini katika maisha. Kitakachokufanya uwe maskini ni matumizi ya mawazo yako katika kukufanikisha.

Wapo watu wengi sana ambao wana kipato kikubwa lakini wanashindwa kufikia utajiri. Hapo hakuna uchawi wowote ni matokeo ya matumizi ya mawazo. Wataalamu wa mambo ya mafanikio wanatuambia hivi, asilimia 90 ya matatizo yote ya pesa yana sababishwa na matumizi ya mawazo au akili zako.

Hivyo, ni muhimu sana kila wakati kuangalia, je mawazo yako yana uwezo wa kukufikisha kule unakotaka kufika kimafanikio? Ukiona una mashaka hata kidogo, ongeza juhudi ya kujifunza na kutamani kujua kila kitu kinachohusiana na pesa na mafanikio maishani mwako.

Wewe ni tajiri mkubwa sana, ikiwa utajiamini na kukubali kutumia nguvu kubwa ya mawazo uliyo ndani mwako kukufanikisha. Miaka kadhaa mbele naamini utakuja kunitafuta na kuniambia aisee ni kweli ulichosema Imani. Yote hayo yanawezekana kwako, hakuna uchawi zaidi kuchukua hatua na kujituma.

Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.

Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
Mawasiliano, Whats app; 0713048035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Iklan Atas Artikel

Iklan Tengah Artikel 1

Iklan Tengah Artikel 2

Iklan Bawah Artikel